Picha: Wasanii wa Kili Music Tour wawalivyowasili Songea
Wasanii watakaopanda jukwaani katika tamasha la ziara
ya Kili Music Tour wamewasili Songea asubuhi ya leo kwa ajili ya
onyesho hilo. Wasanii hao walioongozana na meneja wa Kilimanjaro Premium
Lager, George Kavishe waliwasili kwa ndege maalum wakitokea mkoani
Dodoma ambako jana walishiriki shughuli ya kitaifa iliyoandaliwa na Rais
Jakaya Mrisho Kikwete. Baada ya kuwasili uwanjani moja kwa moja ya
wasanii hao walienda Jogoo FM ambako walifanyiwa mahojiano kabla ya
kwenda uwanjani kufanya majaribio ya sauti na jukwaa na baadae kwenda
hotelini kwa ajili ya kupumzika kabla ya show kuanza. Hizi ni baadhi ya
picha:

Meneja wa Kilimanjaro Premium Lager George Kavishe alikuwa rubani msaidizi

Henry Mdimu aliamua kuonyesha anavyomsubiria kwa hamu Shilole

Linex akishuka kwenye ndege

Malkia Khadija Kopa akishuka kwenye ndege iliyowaleta wasanii toka Dodoma

Mwasiti akishuka kwa umakini ngazi za ndege

Diamond Platnumz akiteta jambo na Ommy Dimpoz huku akishuka kwenye ndege

Pozi kwa pozi kwenye ngazi za ndege

Shilole

Ben Pol akipokelewa na Innocent Nganyagwa ambaye ndiye msimamizi wa wasanii katika
Kili Tour

Gnako Warawara
Safari ya kutoka nje ya uwanja

Mwasiti akiwaongoza wenzake kutoka nje ya uwanja


Diamond akitoka jengo la abiria waliowasili

GNako akiingia ndani ya Tour Bus

Linex

Ben Pol Akiingia kwenye basi

Nikkki wa Pili na wasanii wengine ndani ya Jogoo FM

Ommy Dimpoz akihojiwa ndani ya Jogoo FM










































